Shirika la Ndege la Uganda limezindua safari za ndege za moja kwa moja kati ya mji wa Entebbe, Uganda na mji mkuu wa Somalia Mogadishu. Waziri wa elimu wa Somalia Abdullahi Godah Barre amepongeza uzinduzi huo na kusema Uganda ni nchi maarufu kwa wasomalia wanaotafuta fursa za elimu, na safari za ndege za moja kwa moja zitaimarisha mahusiano kati ya nchi hizo mbili. Ameongeza kuwa kuingia kwa mashirika ya kimataifa ya ndege kunathibitisha kuwa Somalia imeimarisha amani na usalama, na kufungua mlango kwa biashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |