Rais Xi Jinping wa China amehudhuria sherehe ya ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Dunia la Mpira wa Kikapu FIBA kwa mwaka 2019 hapa Beijing.
Akizungumza kwenye sherehe hiyo, rais wa FIBA Horacio Muratore amesema mashindano ya kombe hilo kwa mwaka huu yatakuwa makubwa zaidi na yatatazamwa na watu wengi zaidi katika historia. Ameipongeza China kwa kufanya maandalizi hayo na kusema ana imani kuwa safari hii mashindano ya kombe hilo yatakuwa na mafanikio makubwa.
Kwa mujibu wa mwaliko wa Bw. Muratore, rais Xi alitangaza kufunguliwa kwa mashindano ya kombe la dunia la mpira wa kikapu kwa mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |