• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Kenya azipongeza timu za Kenya kwa kufanya vizuri

    (GMT+08:00) 2019-09-01 17:13:15

    Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amezipongeza timu za Kenya zinazoshiriki michezo mbalimbali ya kimataifa kwa kufanya vizuri.

    Kenyatta amesema amekuwa akifuatilia kwa karibu namna timu za wanawake na wanaume zinavyotawala kwenye michuano na kuongeza kuwa amevutiwa zaidi na uchezaji wa timu za Kenya zilizoshiriki kwenye michauno ya 12 ya All African Games iliyofanyika huko Rabat, Morocco. Kenya imekuwa ya saba katika michuano hiyo ikiondoka na medali 11 za dhahabu, 10 za fedha na 10 za shaba.

    Kwa mujibu wa rais Kenyatta ushindi uliopatikana Ijumaa na timu ya mpira wa wavu ya Kenya Malkia Strikers, umeonesha moyo wa upambanaji wa watu wa Kenya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako