Spurs ilipata bao lake la kwanza kupitia Christian Eriksen baada ya kipa wa Arsenal, Bernd Leno kushindwa kuokoa mpira. Mshambuliaji Harry Kane alifunga bao la pili la Spurs kwa mkwaju wa penalti baada ya Granit Xhaka kumchezea vibaya Son Heung-min katika eneo la hatari.
Arsenal ilipata bao lake la kwanza kabla ya mapumziko kwa Alexandre Lacazette aliyewatoka mabeki wa Spurs na kupiga shuti lililomshinda kipa Lloris na kujaa nyavuni.
Dakika 20 kalba mpira kumalizika, mshambuliaji Pierre Emerick Aubameyang aliisawazishia Arsenal akiunganisha shuti lililopigwa na Guendouzi.
Mchezo mwingine ulikuwa baina ya Everton iliyowachabanga Wolverhampton kwa magoli 3-2.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |