Mshauri wa rais wa Syria Buthaina Shabaan amesema usitishaji vita uliotangazwa hivi karibuni na jeshi la Syria katika mkoa wa kaskazini magharibi wa Idlib ni "wa muda".
Vyombo vya habari jana vilimnukuu Bw. Shabaan akisema kuwa, uamuzi huo wa kusimamisha vita ulioanza kutekelezwa Jumamosi ni wa upande mmoja wa Russia na Syria, na si sehemu ya maelewano mengine yoyote yale.
Bw. Shabaan amesema, jeshi la Uturuki ambalo limeingia kwenye sehemu za Idlib, "litalazimishwa" kuondoka Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |