Habari hizo zilianza kuenea jana Jumatatu kufuatia kuwa na msimu mzuri wa mwaka 2018/19 kwa makocha hao. Kwa upande wake Klopp alifanikiwa kunyakuwa taji la Champions League akiwa na Liverpool kwa kumfunga Tottenham jijini Madrid baada ya Mauricio Pochettino kuifikisha Spurs katika hatua hiyo ya fainali kwa mara yake ya kwanza.
Wakati kwa upande wa Guardiola ameiongoza Man City kunyakuwa taji la ligi kuu ya Uingereza (EPL) mara mbili mfululizo baada ya kuizidi Liverpool kwa kujivunia point 98.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |