• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bondia Mtanzania atwaa taji la WBO baada ya kumtwanga Zulipikaer Maimaitiali wa China kwa KO, mapokezi makubwa yaandaliwa

    (GMT+08:00) 2019-09-03 10:30:29
    Bondia Mtanzania, Abdallah Shaaban Pazi anayejulikana zaidi kama Dullah Mbabe, amefanikiwa kutwaa taji la WBO -Asia Pacific uzito wa kati baada ya kumpiga kwa Knockout (KO) raundi ya tatu mwenyeji, Zulipikaer Maimaitiali ukumbi wa TSSG Center mjini Qingdao, China.

    Dullah Mbabe alilianza pambano kwa kasi na kumpelekea makonde mfululizo Zulipikaer, bondia namba moja China ambaye ndiye aliyekuwa anashikilia mkanda huo, kabla ya kumkalisha chini raundi ya tatu.

    Promota wa Dullah Mbabe, Jay Msangi amesema maandalizi kabambe yanaandaliwa nchini Tanzania kumpokea bondia huyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako