• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Blick arejea kwa kishindo

    (GMT+08:00) 2019-09-03 10:30:52
    Dereva mahiri wa Uganda Arther Blick Jr akishirikiana na mwenzake George Ssemakula wameshinda ubingwa wa taifa wa shindano la magari nchini humo.

    Wakitumia gari aina ya Mitsubishi Evo X, walimaliza mbio hizo za magari kwa kutumia saa 01:12:53 wakifuatiwa na Alwi Hassan akiwa na dereva mwenzake Siraj Kyambadde wakikamata nafasi ya pili kwa kutumia gari aina ya Subaru N14, walitumia saa 01:13:24 huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na madereva Yasin Nasser akishirikiana na Ali Kitumba waliokuwa na Subaru GVB na walimaliza kwa kutumia saa 01:13:34.

    Wakizungumza mara baada ya kushinda, Blick alisema, shindano lilikuwa gumu kutokana na madereva wote kuwa na uzoefu na walimhofia zaidi Alwi Hassan.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako