• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda: Umeme yaunganisha wateja 93,580 Uganda

    (GMT+08:00) 2019-09-03 19:25:07
    Kampuni ya kusambaza kawi nchini Uganda Umeme imesajili ukuaji wa asilimia 7.2 katika viunganisho vya wateja huku 93,580 wakiunganishwa katika nusu ya kwanza ya 2019.

    Takwimu kutoka kwa kampuni hiyo zinaonyesha kuwa wateja 93,580 wameunganishwa kwenye gridi ya taifa ikilinganishwa na 82,373 iliyounganishwa katika kipindi kama hicho mwaka jana.

    Inasema ripoti hiyo kwamba viunganisho kwa jumla vilikua kwa asilimia 7.2 kwa kipindi cha miezi sita iliyopita na kuongeza wigo wa wateja hadi 1.4.

    Hata hivyo idadi ya wateja wapya iko chini kuliko lengo la serikali, ambalo mnamo Novemba mwaka jana ilizindua utekelezaji wa sera ya uunganisho wa umeme bila malipo kwa lengo la kuunganisha wateja 300,000 kila mwaka.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako