Bunge la Afrika Kusini jana lilitoa wito wa kukomesha mashambulizi yanayosababishwa na chuki dhidi ya wageni wakati wageni wengi zaidi nchini humo wameshambuliwa katika siku kadhaa zilizopita.
Mwenyekiti wa Kamati ya bunge ya biashara na viwanda, maendeleo ya uchumi, maendeleo ya biashara ndogo, utalii, ajira na kazi Mandla Rayi amesema, ni muhimu kwamba vyombo vya utekelezaji wa sheria vijitahidi kuwasaka na kuwakamata washambuliaji na kuchukua hatua ipasavyo ili kukomesha mashambulizi hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |