Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Dkt Damas Ndumbaro amesema Tanzaia imeridhishwa na uamuzi wa mahakama. Hata hivyo mkulima Hermanus Steyn anbaye aliwasilisha kesi hiyo mahakamani na kupata kibali cha kushikiliwa ndege hiyo amesema hajaridhishwa na hukumu hiyo. Ndumbaro amesisitiza kuwa Tanzania tayari imemlipa Steyn dola milioni 20, na wako tayari kumalizia deni lote ila mkulima huyo anatakiwa kurudi katika mahakama za Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |