Mfumo wa Satelaiti za Kuongoza Mawasiliano wa Beidou wa China BDS ni moja ya kampuni nne kubwa zinazotoa huduma za kuongoza mawasiliano kwa satelaiti duniani. Hadi sasa idadi ya satelaiti za mfumo huo imefikia 39.
Naibu mkurugenzi wa Ofisi ya usimamizi wa Mfumo wa Satelaiti za Kuongoza Mawasiliano wa China Bw. Yang Jun ameeleza kuwa, China itarusha satelaiti 5 hadi 7 mwaka huu, na 2 hadi 4 mwaka ujao, ambapo ujenzi wa mfumo wa BDS utakamilika kwa pande zote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |