Timu ya raga ya KCB ya Kenya wanahitaji kufika nusu fainali ya duru ya mwisho ya raga ya kitaifa ya wachezaji saba kila upande ya Drifwood, ili kutangazwa mabingwa wa mwaka huu baada ya kufungua mwanya kwa alama 10 katika msimamo wa ligi hiyo.
KCB wamefikisha alama 94 baada ya kuongeza alama 22 kwenye mchezo wao wa mwisho. Huku timu ya Mwamba yenyewe imesalia nafasi ya pili, na nafasi ya tatu inakaliwa na Nakuru na nafasi ya nne inashikiliwa na Homeboys huku Mengai Oilers iko nafasi ya tano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |