Timu ya mpira wa kikapu ya wanaume ya Mazembe sambamba na timu ya wanawake Makomeno za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR Congo) zimenyakuwa ubingwa wa ligi ya kikapu ya nchini humoi mwaka huu.
Kwenye fainali ya ligi hiyo, Mazembe waliwafunga SCTP Kinshasa 84-59, huku Makomeno wakiwasambaratisha CNSS Kinshasa kwa 60-39.
Mchezaji na mfungaji bora kwa upande wa wanawake ni Marlene Ngobeleza, kwa upande wa wanaume tuzo ya mchezaji bora imekwenda kwa Patrick Buzangu na mfungaji bora Bobo Kasongo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |