• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Ronaldo ashinda tuzo nyingine kubwa

    (GMT+08:00) 2019-09-05 10:53:07

    Cristiano Ronaldo amezidi kujiwekea historia baada ya kutwaa tuzo ya 10 kama mchezaji bora wa mwaka nchini Ureno.

    Ronaldo mwenye umri wa miaka 34, amekuwa akifanya vizuri kwenye tuzo hizo tangu mwaka 2007. Huku akiisaidia klabu yake ya Juventus kutwaa taji la nane mfululizo la Serie A.

    Nyota huyo ametwaa tuzo hiyo kwa kumshinda kinda wa Atletico Madrid, Joao Felix, mchezaji wa Manchester City, Bernardo Silva, kiungo wa Sporting Lisbon, Bruno Fernandez na Ruben Neves wa Wolves.

    Tuzo hizo zimetolewa huko Carlos Lopes Pavilion katika jiji la Lisbon mahala ambapo Ronaldo amekulia wakati alivyokuwa kijana mdogo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako