Timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars imepania kufanya vyema katika mchezo wake wa kirafiki wa kimataifa utakaowakutanisha na majirani zao Uganda Cranes uwanjani MISC Kasarani mwishoni mwa wiki hii.
Chini ya kocha mpya Francis Kimanzi, Harambee Stars wanatumia mchuano huo kama sehemu ya mikakati ya kujiandaa kwa kivumbi cha kufuzu kwa fainali za Kombe la Afrika (AFCON) 2021 nchini Cameroon.
Kwa Uganda, mechi hiyo itawapa jukwaa la kujinoa kwa mchujo wa mikondo miwili ya kufuzu kwa CHAN 2020 dhidi ya Burundi na AFCON 2021.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |