Shirikiso la mpira wa miguu nchini Zambia (FAZ), limeliandikia barua Shirikisho la mpira wa miguu la Afrika Kusini (SAFA) ikiiarifu lengo la kufuta mechi ya kimataifa ya kirafiki baina yao na Timu ya Bafana Bafana iliyotarajiwa kuchezwa Jumamosi hii katika dimba la National Heroes, jijini Lusaka, Zambia kutokana na hali ya machafuko yanayoendelea nchini humo.
Kutokana na taarifa hiyo ya kusitishwa kwa mechi na Zambia Wanachipolopolo, shirikisho la mpira wa miguu Afrika Kusini (SAFA) limeanza mchakato wa kusaka timu nyingine ya kucheza nayo kutokea ukanda wa COSAFA ambayo itakuwa tayari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |