Timu ya taifa ya wanawake ya DR Congo (Leopards Dames) itacheza na timu ya taifa ya wanawake ya Cameroon kati ya Septemba 27, 28 au 29 katika mchezo wa raundi ya tatu ya hatua ya makundi kufuzu michuano ya kombe la dunia kwa wanawake.
DR Congo ilifuzu hatua hiyo kwa kupata mteremko baada ya timu ya taifa ya Equatorial Guinea kujiondoa kwenye michuano hiyo. Cameroon yenyewe imeingia hatua hiyo baada ya kuiondoa Ethiopia.
Michezo mingine itakuwa kati ya Ivory Coast itakayokutana na Nigeria, Ghana watakipiga na Kenya, huku Zambia wenyewe watavaana na Botswana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |