Dirisha dogo la usajili limefungwa Jumatatu wiki hii, nyota wa kimataifa raia wa Brazil na mchezaji wa PSG, Neymar da Silva Santos Jr, alikuwa njiani kurudi Uhispania katika klabu yake ya zamani Barcelona, lakini ghafla uhamisho huo umeota mbawa.
PSG walipanga kumuuza Neymar kwa dau ambalo hawakutaka kulipunguza, huku wakipuuza maombi ya mchezaji mwenyewe, na kukaa kibiashara zaidi. Kutokana na dau kubwa, PSG wameshindwa kumuuza Neymar na hivyo kusalia katika klabu hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |