Maseneta wamehiari kuchukua Sh316.5 bilioni zilizo kwenye nakala mpya ya Mswada wa Ugavi wa Raslimali ambao ungali kwenye kamati ya mazungumzo baina ya bunge la seneti na bunge la kitaifa.
Kiongozi wa Wengi katika Seneti, Kipchumba Murkomen amesema wamefikia uamuzi huo mgumu ili kunusuru serikali za kaunti ambazo kupitia kwa baraza la magavana zilitishia kufunga shughuli mwezi huu wa Septemba.
Magavana wamekuwa wakitaka wapewe takribani Sh335 bilioni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |