Timu za Misri na China zimetangaza kuanza kutekeleza mradi wa satelaiti unaofadhiliwa na China. Mwezi Januari, Misri na China zilisaini makubaliano kuhusu China kuchangia dola za kimarekani milioni 72 kwenye mradi huo wa satelaiti ya "MisrSat II", ambayo ni satelaiti ndogo ya hali ya juu ya kuhisi kwa mbali. Misiri inaona kuwa mradi huo ni ushirikiano mwingine mkubwa kati ya nchi hizo mbili kwenye shughuli ya anga ya juu, baada ya kusaini makubaliano ya kujenga kituo cha kuunda na kufanyia majaribio satelaiti nchini Misri, ambacho kinatarajiwa kuzinduliwa mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |