Wizara ya ulinzi ya Uturuki imesema nchi hiyo na Marekani zimeanza kufanya doria ya pamoja katika Eneo Salama kaskazini mwa Syria. Doria hiyo ni sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa Agosti 7 kati ya washirika hao wawili wa NATO. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Eneo Salama na njia ya amani vitaundwa kaskazini mwa Syria na kuondoa wasiwasi wa Uturuki juu ya kikundi cha Wakurdi kinachodhibiti sehemu hii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |