Msemaji wa ofisi ya waziri mkuu wa Uingereza jana alisema, baada ya kuikataa ajenda ya waziri mkuu, bunge la Uingereza litafungwa kuanzia usiku wa siku hiyo hadi Oktoba 14.
Inaaminika kuwa bunge la Uingereza jana liliipigia kura ajenda ya uchaguzi mkuu iliyotolewa na serikali kwa mara ya pili. Vyama vya upinzani kikiwemo chama cha Labour vilisema havitaunga mkono ajenda hiyo, ili kuhakikisha Uingereza haijitoi kwenye Umoja wa Ulaya bila makubaliano. Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson tarehe 4 aliwasilisha ajenda bungeni na kutoa ombi la kufanya mapema uchaguzi mkuu tarehe 15 mwezi Oktoba, lakini ajenda hiyo haikupitishwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |