Jengo linaloaminiwa kubwa zaidi duniani la kuhudumia shughuli za uwanja wa ndege (jengo la satilaiti) linatarajiwa kuanza kutumiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Pudong, Shanghai tarehe 16, Septemba. Likiwa kusini mwa majengo mawili ya abiria ya sasa, jengo hilo litatoa huduma kwa abiria kupanda, kushuka na kubadili ndege. Abiria wanaweza kusafiri kati ya majengo makuu ya abiria na jengo la satilaiti kwa treni ya mwendo kasi kwa dakika 2.5 tu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |