Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Fedha la Kimataifa IMF imetangaza kuwa itafikiria kumteua Kristalina Georgieva kutoka Bulgaria ambaye sasa ni ofisa mkuu mtendaji wa Benki ya Dunia kuwa mkurugenzi mkuu wa IMF. Georgieva, aliyeteuliwa na Umoja wa Ulaya kuongoza IMF amekuwa mteuzi pekee wa nafasi hiyo kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kuwasilisha majina ya wateuzi Ijumaa iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |