Takwimu zilizotolewa leo na Idara ya takwimu ya China zinaonyesha kuwa kiwango cha bei ya bidhaa za walaji ya China CPI kimeongezeka kwa asilimia 2.8 mwezi Agosti, kiasi ambacho ni sawa na mwezi uliopita.
Takwimu zinaonyesha kuwa katika mwezi Agosti, bei ya chakula iliongezeka kwa asilimia 10.0, na bei ya bidhaa zisizo chakula imeongezeka kwa asilimia 0.1. Zaidi ya hayo, kiwango cha gharama za uzalishaji wa bidhaa za viwandani cha China PPI kilipungua kwa asilimia 0.8 mwezi Agosti.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |