Zanzibar inapigia nchi yake debe kwa wawekezaji wa kimataifa kutokana na kukua kwa kasi kwa sekta ya utalii.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein amesema kuwa kisiwa hicho, pamoja na bahari nzuri zinafasi nzuri ya kushindania faida za utalii na nchi zengine za Afrika Mashariki.
Aidha amesema kuwa serikali yake inaangalia kuvutia wawekezaji wengi katika hoteli na utalii kwani kisiwa kinataka kuwa na ushindani zaidi.
Zaidi ya watalii 520,800 walitembelea kisiwa hicho mwaka jana, na kufanya, utalii kuwa sekta inayoongoza kwa uchumi kwa Zanzibar.
Kisiwa hicho sasa kinapata zaidi ya dola milioni 312 kutoka kwa utalii kila mwaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |