Makamanda wa majeshi ya Uturuki na Marekani wamefanya mazungumzo mjini Ankara juu ya eneo salama litakaloanzishwa nchini Syria na majadiliano yao yataendelea katika Kituo cha Operesheni ya pamoja wilayani Akcakale, kusini mwa mkoa wa Saliurfa. Kamandi ya Marekani kwa Ulaya (USEUCOM) imesema makamanda hao watajadili msaada zaidi kwa Kituo hicho na shughuli nyingine muhimu zitakazohimiza maendeleo na usimamizi wa utaratibu wa usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |