Jack Ma amestaafu rasmi kama mwenyekiti wa kampuni ya Alibaba na kukabidhi nafasi hiyo kwa Mkurugenzi mkuu mtendaji wa kampuni hiyo Daniel Zhang. Katika barua yake aliyotoa kwa umma Septemba, 10, mwaka jana, bilionea huyo ambaye pia ni mwanzilishi wa kampuni hiyo kubwa ya biashara ya mtandaoni alisema Alibaba kamwe haimilikiwi naye peke yake, lakini atakuwa nayo daima.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |