Rwanda, Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR na Umoja wa Afrika wamesaini hati ya maelewano (MoU) kuhusu kuanzisha utaratibu wa mpito wa kuondoa wakimbizi na watafuta hifadhi kutoka Libya. Awamu ya kwanza ya wakimbizi na watafuta hifadhi 500 wataondolewa katika wiki kadhaa zijazo.
Kwa mujibu wa makubaliano haya, Rwanda itapokea na kuwalinda watu hao pamoja na wengine waliotambuliwa kuwa wanyonge na walio hatarini ambao sasa wanashikiliwa katika vituo vya mahabusu nchini Libya, na watahamishiwa kwenye maeneo salama nchini Rwanda kwa hiari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |