Serikali ya Algeria imeamua kufuta kanuni kuhusu uwekezaji ili kuvutia uwekezaji mwingi zaidi wa kigeni. Chaneli ya televisheni ya Echorouk ya Algeria imesema, baraza la mawaziri linaloongozwa na waziri mkuu Bw. Noureedine Bedoui limeamua kufuta sheria ya 49/51 inayohusiana na uwekezaji wa kigeni, ambayo ilipitishwa katika sheria ya bajeti ya mwaka 2009 kutoa kiwango cha juu cha hisa katika miradi ya ushirikiano kwa waalgeria
Kanuni hiyo ilikosolewa mara nyingi na makampuni ya kigeni na wataalamu wa uchumi, ambao walisema imezuia maendeleo ya uchumi wa taifa kwa kuwazuia waendeshaji wa kigeni kuwekeza nchini Algeria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |