Maonyesho ya kwanza ya kimataifa ya vipuri vya magari ya Zhejiang yamefunguliwa mjini Nairobi, Kenya. Makampuni zaidi ya 30 kutoka mkoa wa Zhejiang, China yameonyesha vipuri vyao vyenye ubora wa juu.
Katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje ya Kenya, Bw. Ababu Namwamba amesema, maonyesho hayo yamevutia watu elfu 2 kutoka nchi za Afrika Mashariki, ambao wanataka kununua vipuri vya kisasa kabisa kuvumbuliwa katika teknolojia ya magari.
Bw. Namwamba pia amesema, Kenya inapenda kuvutia wawekezaji wa China watakaoiwezesha sekta ya magari ya nchi hiyo kuwa na ushindani katika soko la kikanda na la kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |