• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yaridhia kuondolewa vikwazo dhidi ya CAR

    (GMT+08:00) 2019-09-13 08:53:29

    China imeridhia azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la kuondoa vikwazo vya usafirishaji wa silaha dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR. Naibu mwakilishi wa kudumu wa China kwenye Umoja wa Mataifa Wu Haitao amesema China inaunga mkono kuondoa vikwazo hivyo na hatua nyingine dhidi ya CAR kwa mujibu wa hali halisi ya nchi na matarajio ya serikali ya CAR. Ameliambia Baraza la Usalama kuwa hali ya jumla nchini humo imeboreshwa, na serikali ya CAR imeahidi kutekeleza makubaliano ya amani na maelewano, hali hizo chanya zimekidhi kigezo cha Baraza la Usalama cha kupitia upya vikwazo hivyo vya usafirishaji wa silaha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako