Wanigeria wasiopungua elfu 22 wameripotiwa kutojulikana walipo tangu kundi la Boko Haram kuanza mashambulizi yake miaka kumi iliyopita katika sehemu za kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu ICRC Peter Maurer aliye ziarani nchini Nigeria amesema idadi hiyo ni kubwa zaidi kuliko nchi yoyote nyingine iliyorekodiwa na ICRC, na kuongeza kuwa asilimia 60 ya watu waliopotea ni watoto, hali inayoonyesha kuwa maelfu ya wazazi hawafahamu watoto wao walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |