Jumla ya watalii milioni 105 wa China wamesafiri maeneo mbalimbali nchini katika mapumziko ya siku tatu ya sikukuu ya mbalamwezi iliyoanza Ijumaa na kumalizika Jumapili. Ikitoa takwimu hizo wizara ya Utamaduni na Utalii imesema idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 7.6 ikilinganishwa na sikukuu ya mwaka uliopita. Shughuli hizi za utalii zimeingiza mapato ya yuan bilioni 47.28 sawa na dola bilioni 6.7 za kimarekani, ambayo imepanda kwa asilimia 8.7 kuliko mwaka jana wakati kama huu. Sikukuu ya mbalamwezi inaadhimishwa kwa shughuli mbalimbali zikiwezmo kujumuika pamoja kwa familia, kuangalia mwezi mpevu na kula keki ya mbalamwezi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |