Mkutano wa Kimataifa wa kuzuia Unyanyasaji na Kuwapuuza watoto umeanza jana Muscat Oman ukiwa na kauli mbiu "Kuelekea maisha bora ya watoto katika siku za baadaye". Mkutano huo umewaleta pamoja washiriki 400 kutoka nchi na kanda 35. Kwenye makala yake ya sita, mkutano huo utaangalia mitandao ya kijamii, uonevu, unyanyasaji, utelekezaji, na sababu ya matukio makubwa. Kulingana na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano Mona Fahad Ali Said, mkutano huo unalenga kuamua mipango ya baadaye ya kuwalinda watoto na hatari za manyanyaso.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |