Umoja wa Afrika umelaani shambulizi dhidi ya askari wa Burundi wa tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia. Shambulizi hilo linalodaiwa kufanywa na kundi la al-Shabab, limesababisha vifo na majeruhi ya askari ambao walikuwa kwenye msafara.
Mwenyekiti wa Umoja w Afrika Bw. Moussa Faki Mahamat amelaani shambulizi lililotokea jumamosi iliyopita huko Hirshabelle, na kutoa salamu za pole kwa familia za watu waliouawa na serikali ya Burundi na kuwatakia majeruhi wapone haraka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |