Wizara ya kilimo nchini Kenya imedinda kuidhinisha uagizaji wa mahindi ya manjano hali inayoweza kusababisha ushindani wa mahindi nyeupe.
Kwa kawaida wasagaji wa lishe za mifugo huagiza mahindi ya manjano kwa ajili ya uzalishaji wao.
Eneo la Bahari Nyeusi ambako mahindi hayo yalikuwa yanapitia limefungwa, na sasa iwapo serikali itaidhinisha uagizaji upya wadau watanunua kutoka Ukraine.
Mwenyekiti wa Chama cha lishe la mifugo nchini humo Joseph Karuri amesema wamewasilisha swala hilo kwa katibu wa kudumu wa wizara ya kilimo na kwamba wamekuwa katika mazungumzo naye.
Wasagaji pia wanaomba kuruhusiwa kuagiza mtama mweupe kutoka Amerika na tayari wamefanya mazungumzo na baraza la Nafaka la Amerika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |