• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uwekezaji wa moja kwa moja Afrika Mashariki waongezeka

    (GMT+08:00) 2019-09-18 19:38:13

    Ukuaji endelevu wa uchumi kati ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki umeendela kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

    Ripoti ya kampuni ya ukaguzi ya Ernst & Young (EY) inasema kwamba ukuaji wa ndani unaongezeka kwa asilimia saba nchini Kenya, Uganda, Rwanda, Tanzania na Ethiopia huku ukivutia wawekezaji kwenye kanda hiyo na, na kufunngua nafasi nyingi za ajira.

    Kwa jumla kanda ya Mashariki mwa Afrika ina uchumi wa thamani ya dola bilioni 265, na linakadiriwa kuwa na ushawishi mkubwa katika kuvutia wawekezaji katika muongo mmoja ujao.

    Hata hivyo licha ya ugunduzi wa amana kubwa za mafuta, gesi na madini mengine, wawekezaji wa kigeni wanawekeza sana kwenye sekta za rejareja, fedha, simu, teknolojia, huduma ya biashara na burudani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako