• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Mechi za ligi ya Mabingwa Ulaya-Madrid yaonja muziki wa PSG, Bayern yapeta

    (GMT+08:00) 2019-09-19 08:59:03

    Ligi ya mabingwa Ulaya imeendelea jana kwa michezo kadhaa katika viwanja tofauti, kundi A, Paris Saint Germain imewapiga bila huruma Real Madrid goli 3-0, huku Galatasaray ikilazimishwa sare na Club Bruggle. Kundi B imezikutanisha Olympiacos iliyomaliza kwa sare ya 2-2 na Tottenham Hotspurs, huku Bayern München ikiilaza FK Crvena Zvezda goli 3-0. Na katika kundi C, Dinamo Zagreb imeifurumishia mvua ya magoli 4-0 Atlanta, nayo Shakhtar Donetsk imekubali kichapo cha goli 3-0 toka kwa Manchester City. Michezo ya mwisho ilikuwa ni kundi D, Atletico Madrid imetoshana nguvu ya goli 2-2 na bibi kizee wa Turin Juventus, nao Lokomotiv Moscow ikiimaliza Bayer Leverkusen kwa goli 2-1.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako