Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema vyama vyote muhimu nchini Syria vimefikia makubaliano juu ya muundo wa kamati inayoshughulikia kurekebisha katiba ya nchi hiyo.
Guterres amesema mjumbe wake maalumu nchini Syria Geir Pedersen anafanya "kazi ya mwisho", na kwamba wanatumaini kuwa itakamilika mapema, na pia itakuwa hatua muhimu katika kujenga mazingira kwa ajili ya ufumbuzi wa kisiasa kwa mgogoro wa Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |