Rais wa zamani wa Ufaransa Bw. Jacques Chirac amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 86. Mwanasiasa huyo wa mrengo wa kulia na kati alikuwa anajulikana zaidi kwa kuamua kupinga operesheni ya kijeshi dhidi ya Iraq ya mwaka 2003 iliyoongozwa na Merekani. Uamuzi huo ulimletea heshima nchini mwake, lakini ulidhuru uhusiano wa kidiplomasia kati ya Ufaransa na Marekani. Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo amefuta mpango wake wa kutembelea kusini magharibi mwa nchi hiyo, na atahutubia wananchi kupitia televisheni kuhusu kifo cha Chirac.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |