Waziri mkuu wa Uingereza Bw. Boris Johnson jana ameanzisha mjadala kuhusu Uingereza kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya (Brexit), akisema kuwa Uingereza itaondoka Umoja wa Ulaya mwezi ujao licha ya azimio la bunge linalomlazimisha kutafuta kuahirisha mchakato huo iwapo makubaliano yoyote hayatafikiwa.
Katika ufunguzi wa mkutano huo, mawaziri walitoa hotuba ya kuunga mkono uamuzi wa Bw. Johnson kuhusu kumaliza uanachama wa Uingereza kwenye Umoja wa Ulaya itakapofika Oktoba 31.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |