• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • East African Itakuwa msimu mgumu wa chai kwa wakulima wa Afrika Mashariki, kufuatia kushuka kwa bei katika soko  za Kimataifa

    (GMT+08:00) 2019-10-02 19:52:28

    Itakuwa msimu mgumu wa chai kwa wakulima wa Afrika Mashariki, kufuatia kushuka kwa bei katika soko za Kimataifa kutoka dola 2.98 kwa kilo mwaka 2017 hadi dola 1.76 kwa kilo mwezi Julai.

    Uzalishaji wa chai ya kimataifa mnamo 2018 ulikadiriwa kuwa kilo bilioni 5.85 kutoka kilo bilioni 5.81 mnamo 2017, ongezeko la asilimia 0.68 huku mchango wa Afrika ukisimama kwa kilo milioni 717.

    Jumla ya mauzo ya nje yalikuwa kilo bilioni 1.8, huku Afrika ikichangia kilo milioni 654 kwa asilimia 35.

    matumizi ya dunia yaliandikisha ongezeko la asilimia 2.4 kwa kilo bilioni 5.6 ikilinganishwa na kilo bilioni 5.4 mnamo 2017.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako