Wafanya biashara hao wadogo walio na vibanda vya mboga eneo la Likoni na wahudumu wa usafiri wa umma walilalamika wakisema hatua hiyo imesitisha kabisa biashara zao,na kuwafanya kupoteza maelfu ya pesa.
Aidha walisema serikali ingefaa kufungua kivuko cha Mtongwe huku shughuli za uopoaji miili zikiendelea katika kivuko cha Likoni.
Kituo cha feri cha Mtongwe kilifungwa Agosti 2019 na kinatazamiwa kurudia shughuli zake Machi 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |