Mchezo wa Ligi ya Europa kati ya F91 Dudelange na FK Qarabag ulisitishwa kwa muda baada ya droni kuonekana kuruka kwenye uwanja. Mchezo huo ulisimama kwa dakika 15 kufuatia kuonekana kwa droni iliyobeba bendera. Wachezaji wa Dudelange na Qarabag, za Azerbaijan, walijaribu kuishusha chini droni hiyo kwa kuipiga kwa mpira. Tukio hilo lilitokea katika kipindi cha kwanza cha mtanange ulioshuhudia Qarabag wakishinda 4-1. Mlinda mlando wa Bosnia-Herzegovina Asmir Begovic, ambaye yupo kwa mkopo kwenye klabu ya Bournemouth iliyopo kwenye Premier League ya Uingereza hadi Januari alikuwa akilinda lango la Qarabag.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |