Polisi mjini London wamesema watu karibu 300 wamekamatwa katikati ya mji huo katika siku ya kwanza ya maandamano ya umma yaliyoitishwa na kundi la Extinction Rebellion, linalotaka kuchukuliwa kwa hatua zaidi za dharura dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. Kundi hilo limesema maandamano hayo makubwa yataendelea kwa wiki mbili. Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson ametaka polisi kutumia kikamilifu sheria dhidi ya waandamanaji hao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |