• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Shirika la ndege la Uganda laongeza ndege mbili

    (GMT+08:00) 2019-10-08 18:56:44

    Shirika la ndege la Uganda limeongeza ndege mbili zaidi ili kuliwezesha kupanua oparesheni zake kusini na kati mwa Afrika.

    Mshauri wa kiufundi wa shirika hilo Cornwell Muleya amesema sasa wathudumu katika miji ya Kinshasa, Asmara, Hergeisa, Lusaka, Harare, Johannesburg, Djibouti na Addis Ababa.

    Shirika la ndege la Uganda lilisitisha oparesheni zake miaka 20 iliopita lakini kuanzisha upya mwezi Agosti baada ya kuanza kununua ndege mpya.

    Kabla ya ndege mbili mpya lilikuwa linahudumu katika miji ya Nairobi, Mogadishu, Juba, Arusha, Dar es Salaam na Mombasa.

    Muleya amesema kwa sasa shirika hilo bado linafadhiliwa na serikali lakini litaanza kuzalsiha faida hivi karibuni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako