• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China na Pakistan zaahidi kuimarisha ushirikiano kati yao

    (GMT+08:00) 2019-10-09 09:04:22

    Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang na mwenzake wa Pakistan Bw. Imran Khan, jana walifanya mazungumzo hapa Beijing na kukubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zao. Bw. Li amesema China inatoa kipaumbele kwenye uhusiano kati yake na Pakistan, na iko tayari kushirikiana na Pakistan kuhimiza uhusiano na ushirikiano ufikie kwenye kiwango kipya. Bw. Khan ambaye yuko Beijing kuhudhuria sherehe ya ufungaji wa Maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo cha Maua Mwaka 2019 na kufanya ziara ya kikazi nchini China, ameshukuru msaada na uungaji mkono wa China, na kusema nchi yake inapenda kuimarisha ushirikiano na China ili kuongeza kasi ya ujenzi wa pamoja wa Ukanda Mmoja, Njia Moja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako