Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekaribisha kuanzishwa kwa Kamati ya Katiba nchini Syria, iliyotangazwa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres Septemba, 23. Baraza hilo limesema kuanzishwa kwa Kamati ya Katiba yenye ridhaa na kuongozwa na waSyria, kunatakiwa kuwa mwanzo wa mchakato wa kisiasa wa kumaliza mgogoro wa Syria. Baraza limesisitiza uungaji mkono wake kwa mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria Bw. Geir Pedersen na pendekezo la Umoja wa Mataifa la kufanya mkutano wa kwanza wa Kamati ya Katiba mjini Geneva Oktoba, 30.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |